Matthew 19:1-6

Isa Afundisha Kuhusu Talaka

(Marko 10:1-12)

1 aIsa alipomaliza kusema maneno haya, aliondoka Galilaya, akaenda sehemu za Uyahudi, ng’ambo ya Mto Yordani. 2 bUmati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akawaponya huko.

3 cBaadhi ya Mafarisayo wakamjia ili kumjaribu, wakamuuliza, “Ni halali mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”

4 dAkawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo mwanzo Muumba aliwaumba mwanaume na mwanamke, 5 enaye akasema, ‘Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja’? 6 fHivyo si wawili tena, bali mwili mmoja. Kwa hiyo alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”

Copyright information for SwhKC